Mimi Na Angola

MIMI NA ANGOLA ni historia ya kweli ya maisha ya mwanaswahiliwood susan natasha humba zamani alijulikana kama susan lewis natasha.

Fuatilia kisa hiki cha kusisimua……

…..ilikuwa ni miezi michache imepita toka nilipofanya kosa kubwa sana lililobadilisha maisha yangu yote. kosa ambalo si tu lilinifanya kujuta na kujiona kama sina thamani  tena maishani, lakini pia ni kosa lililonitoa eneo  moja na kunipeleka eneo jingine. Sikuweza kujitoa kwa vile maji yakimwagika hayazoleki kwa hiyo ilibidi niwe mpole na kukubali matokeo.


Siku isiyo na jina, baba yangu mzee Ngatwika alirudi nyumbani toka kazini akionyesha furaha na kuwa ana neno la kusema, mimi na mama ilibidi tukae kimya kumsikiliza baada ya kupata chakula cha jioni .

“nimepata uhamisho wa kwenda Angola, natakiwa niwe nimeripoti ubalozini ndani ya miezi miwili toka sasa”

Wote tulillipuka kwa furaha na baada ya sekunde kadhaa wote tulibaki kimya huku kila mmoja akizama kwenye mawazo yake binafsi.

Sijui mama na baba walikuwa wakiwaza nini ila kwa upande wangu nilijiona kuwa nina bahati mbaya maana kama nilivyosema hapo awali ilikuwa ni miezi michache toka nimetenda kosa kubwa maishani na kosa lenyewe linaweza kunifanya nisiende hii safari tofauti na safari zote wanazokwenda wazazi wangu,

ni kosa gani hilo alilofanya Susan linalomyima raha? Huo ni mwanzo tu wa tamthilia hii tamu ya simulizi, endelea kufuatilia ujue 

Monalisa Tanzania

Hi! karibu katika blogsite yangu ya Monalisatanzania. upate kunifahamu japo kwa ufupi na kipekee kama shabiki au mpenzi wa kazi zangu. utapata habari, burudani na taarifa official kutoka kwangu. enjoy!

Mpya zaidi Nzee zaidi