Behind the scenes: HOMECOMING

SEKO SHAMTE ni mwanadada wa kitanzania aliyeamua kuingia katika tasnia ya filamu kwa namna nyingine na ya kipekee zaidi; akitengeneza na kutoa filamu zenye ubora wenye unaoelekea hadhi ya kimataifa zaidi. yawezekana halizingatii soko la filamu pale kariakoo, au ana mtazamo mwingine wa kipekee zaidi.  ]hayo yote na mengineyo nitawaletea siku nyingine, lakini kwa sasa, hembu tufurahishe vichwa vyetu kwa kujifunza kuhusu filamu kwanza.
Kama umebahatika kuona tamthilia ya THE TEAM utakubaliana nami pia namna kazi za Director huyu mwanadada anayepata umaarufu wake katika kazi za filamu kwa kasi,  ila utakapobahatika kuitazama au kuiangalia filamu ya HOMECOMING utaelewa ni jinsi gani alivyoamua kwenda next level.
Hapa nitaongelea yaliyotokea behind the scene nikiwa kama mmoja wa waigizaji niliyeigiza kwa jina la auntie Rehema, mke wa waziri mstaafu mhe. Mshindi (hashim kambi) ingawa jina langu halisi ni Susan natasha Humba.
ENjoy!



Nimecheza kama Auntie Rehema, Mke wa waziri mstaafu Mh. Mshindi, na pia mlezi wa abel (Daniel kijo) aliekuwa kinara wa filamu ya homecoming.
 Mazoezi ya filamu yalifanyika kwa muda kiasi cha kila mtu kushika mistari yake na kuzoeana na mwenzake. Kwa upande wangu Daniel ilikuwa ni mara ya kwanza kukutana nae lakini baada ya dakika chache tulikuwa kama kweli ni mtu na untie yake. kwa upande wa  hashim kambi yeye sikuwa na shida nae nilishaigiza nae filamu nyingi nikiwa kama mkewe .



Starring of the Film, Daniel Kijo. Mtangazaji wa Awali wa vipindi vya Televisheni, 5 Connect (EATV) na Daladala
 Siku ya kwanza ya shooting ilikuwa ni Airport ya Dar es Salaam (Julius  Nyerere International Airport) Ikiwa ni scene ya kumpokea Abel anayerudi toka Marekani.
Directors walikuwa wawili, mmoja toka Africa kusini na mwingine ni mwanadada Seko Shamte akiwa ni director mkuu.  Mpiga Picha D.O.P (director of photograph) alikuwa mmarekani na msaidizi wake wakiwa wanatumia mojawapo ya kamera bora za wakati huu.






Na nyuma yetu likiwepo jopo la watu wengi huku kila mmoja akiwa na kazi yake wako wanaoshika taa na kurekebisha  mwanga, sauti, waya, makeup, maleba, location, madereva n.k
Tulifika pale saa 12 asb na kutoka saa 7 mchana.





BAADA ya hapo goma liliendelea kwa siku 20 mpaka kumalizika shooting nzima.
Nakumbuka scene nyingine niliyoshiriki iliyochukua muda mrefu ni ya sherehe ya kumkaribisha abel aliekuwa amerejea nyumbani tz toka marekani masomoni.
HAPA dada wa makeup alikuwa kazini……


Waswahili wanasema "shida haikosekani kazini" hata siku ya harusi katika bahati mbaya sana kuna kosa lilifanyika ambalo halikuweza kuzuilika, kwani nguo niliyoivaa airport niliondoka nayo sikuiacha kama zile zingine na niliporudi siku nyingine kwa ajili ya scene ya sherehe, ikawa haipo ingawa ilitakiwa. Ikabidi director afanye marekebisho ya chap chap. Pole sana Seko.

Airport nilipompokea Abel nilionekana hivi…..

Na kwenye sherehe ingawa ilikuwa ni siku hiyohiyo (kama inavyosema script)  nilikuwa na muonekano huu….


Ni kosa kubwa sana kwa mwigizaji kuondoka na nguo ya shooting, lakini waswahili wanasema ajali kazini!

Susan Natasha Humba, Mama Abdul na Mama Shela

Shooting iliendelea na waigizaji waalikwa walikuja katika scene hiyo ya sherehe…

Pamoja na waigizaji wengine waliokuwepo mzee chilo alikuwa ni mchumba wangu utotoni (kwenye filamu)



Baba wa Abel katika pozi
pia aliigiza kama baba mzazi wa Daniel kijo abel anaeishi kijijini ambaye alinyanganywa uchumba wangu na Mh. Waziri Mshindi (Hashimu kambi)

scene hii tuliipigia  mabwepande na ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika eneo hilo. Na ujanja wangu woote ila sijawahi kufika eneo hili. (kumbe jiji la Dar ni kubwa namna hii?).
Mapumziko kazini
Kuonyesha wako vizuri kila idara tulikula  vizuri na kunywa.
 kuanzia chai saa 12 asb, chakula cha mchana muda muafaka na vitamtam vya kumwaga  na  after lunch tulipumzika kama hivi.









Huyo mkaka mbele ndie director toka South Africa na huyu mzungu nyuma ni msaidizi wa mpiga picha , nilipewa story yake na d.o.p alifanyaga kituko flani amazing huko kwao, nilicheka sana na kuanzia siku hiyo nilimpachika jina la 'Mr. Trouble-some'.


Kwa upande wangu nimefurahi kufanya kazi na cast na crew wote wa filamu ya homecoming  bila kumsahau muddy niliyekuwa nikimwamsha saa 10 na nusu usiku kwa ajili ya kwenda shooting  kisa eti nampitia! 
Katika filamu kuna scene mbalimbali za mahela  na haya ndio yaliyotumika
 Pia nakupa big up nyingi saaaana sana sanaaaa director Seko Shamte ukiungana na madirector wanawake wenzako, Honeymoon Aljabri wa filamu ya Daddy's Wedding, Leah Mwendamseke alieongoza filamu kadhaa za bongo muvi na Yvonne Cherrly (Monalisa) ambaye pia ameongoza filamu kadhaa ikiwemo chanzo ni mama.



Niliyekuandalia kitu hiki kizuri, Ni mimi mwanaswahiliwood, Sinyora Susan Natasha Humba (kubwa la maadui)
Mpya zaidi Nzee zaidi