MPELELEZI HAUZIWI MCHELE.

MIMI NA ANGOLA


SEHEMU YA TATU


 Nakumbuka siku moja tulikuwa tunacheza jioni maeneo ya kulaza magari mara tukamwona mfanyakazi wa ndani anakuja  akiwa na wasiwasi akatukutanishana  watoto  wote na kutuamuru twenda eneo Fulani mle mle kwenye eneo letu la diplomats na kutuweka pamoja kama vile kuna vita, eneo zima lilikuwa limezizima kwa hofu na sintofahamu.  Baada ya dakika chache tukaruhusiwa kurudi majumbani mwetu na kuambiwa kilichotokea, kumbe umeme ulikatika kwa dakika 2 tu! Sikuwahi kuona umeme ukikatika miaka yote mitano tuliyokaa china!   Tanesco mpo hapo?

Hii ni hadithi ya maisha yangu ikiandikwa na mimi mwenyewe.
Susan natasha humba.
Endelea sura ya nne ya mimi na Angola……


Miaka kadhaa ikapita  tumerudi   Bongo mwaka 1975  ambapo kukatika umeme ni kitu cha kawaida.na mbaya kuliko yote tulikuwa katikati ya miezi kumi na nane ya kujifunga mkanda baada ya vita ya Uganda na Tanzania,ugali wa njano na harage chungu,kila kitu kwa foleni huku magari ya mobile shop yanayuouza unga na bidhaa muhimu ya yakikimbiliwa kila yanapopita mtaani watu kuwahi kuweka mawe kwenye foleni. Ndipo baba alipopata barua ya uhamisho kwenda angola  wakati mchele ulikuwa  ni bidhaa adimu ukienda sokoni tandika unaona punje chache za mchele zimewekwa juu ya gunia,unasimama na kutoa pesa huku ukiwa peke yako bila muuzaji ingawa yuko mahali akikuangalia na kuhakikisha uko peke yako bila polisi au mpelelezi ndipo muuzaji anakuja fasta anachukua pesa  hamna hata salamu  anapotea akirudi anakuja na mchele uwe mzuri au mbaya,kilo imetimia au la,  utajiju.  Tena kwa mtindo huu tukienda sisi watoto tunapata lakini alikuwa akienda mama yangu wanamnyima kisa eti wanamshuku.
“uza uone. Huyu scrurite shauri yako!  (wanadhani mama ni security yaani mpelelezi, ingawa sio kweli kisa eti muonekano wake na pia anavaa miwani)
Katika kipindi hiki kigumu ndipo baba anapoleta habari nzuri kama hii.
“nimepata uhamisho kwenda Angola ……. Hata kama ungekuwa wewe usingefurahi?
Tulikuwa tumekaa kimya kila mmoja akitafakari kwa upande wake kivyake.
Kwa upande wangu nilijiuliza maswali mengi mojawapo likiwa je?  Ntakwenda?   Maana ni kipindi kifupi nimetoka kufanya kosa kubwa  lililobadili mwelekeo wa maisha yangu toka hali ya utoto niliokuwa nayo hadi utu uzima.  
Kifupi ni kwamba nilitoka kujifungua mtoto mzuri wa kike  waswahili wangemwita mwanaharamu, hana baba  na mimi mama yake sina msimamo wowote wa maisha sikuwa na kazi  wala uwezo wa kumlea.
Baada ya kumaliza darasa la saba shule ya msingi temeke nilienda  shule ya sekondari na ufundi bagamoyo  nikasoma kwa miezi michache na kuacha kwa vile  fani nilizozitaka hazikuwepo nilirudishwa nyumbani nisubiri kwenda shule nyingine na wakati huo wa kusubiri nikafanya utundu  mara ya kwanza maishani na kupata mimba.
Hapa nilipo nimempakata mtoto ambae baba yangu alipomwona tu akitoka hospitali alimpenda na  alimpa jina la mpenzi wangu akawa anampenda kuliko kitu chochote duniani akirudi kazini jambo la kwanza ni kumbeba na kumrusharusha na kuuliza ameshindaje. Usiku mtoto alikuwa ni mlizi sana baba huwa anaacha kitanda na kuja kumbembeleza na kunipa ruhusa nikalale kifupi alitujali kama vile sikuwa nimemfanyia kosa lolote.
Asante baba sina cha kukulipa.I love you dad!

Kama vile baba alijua ninachowaza alikata ukimya ule.
“suzy tutakwenda nae,hatuwezi kumwacha na mtoto mchanga hivi au siyo mama? Pia tutaenda na Tony”
(Rose kwa wakati huu alikuwa ameshaolewa na Tony ni mdogo wangu wa mwisho aliezaliwa china)
Mama alikubali moja kwa moja na kuanza maandalizi.  Utata ukatokea lilipotakiwa jina la mtoto kwa ajili ya kuwekwa kwenye passport wote tukawa kimya.baba aliibuka na wazo.
“kwa vile mimi namwitaga mpenzi wangu basi kwa nini tusimwite hilo hilo jina la mpenzi ila kwa   kifaransa  nadhani litafaa  na aitwe cherrie.
Likaonekana ni wazo zuri tukalipitisha jina hilo  akaitwa cherrie ama kwa Kiswahili Sherry.
siku  ya kuondoka ilifika nakumbuka siku hiyo majira ya saa sita ulipikwa ugali wa njano na maharage mekundu chakula ni kichungu kibaya lakini ndio hivyo lazima ule ili usife,gari lilikuja na tukajipakia kuelekea uwanja wa ndege saa nane tulitakiwa kuwasili uwanjani.
Baada ya muda tuliingia ndani ya ndege na kwa kupitia madirisha madogo ya ndege nilikuwa nikiwaangalia ndugu waliokuja kutuaga uwanjani machozi yalikuwa yakinitoka kila nikiwaangalia.
Taratibu ndege ilianza kuondoka huku nikiwaangalia,ilipofika mahali pa kusimama na kuongeza kasi ya injini nililaza kichwa kwenye kiti huku uso ukiangalia mbele sikuangalia tena dirishani huku nimempakata sherry wangu ndege ilianza kuondoka kwa kasi na kuendelea kushika kasi hadi ilipoiacha ardhi na kupaa juu niliendelea kubaki vilevile hadi ilipokaa sawa.
Saa mbili baadae ndege ilitua katika uwanja wa ndege wa Zambia na abiria wote tukashuka  na kuelekea hotelini pale tulikuwa tunatakiwa kesho kushinda kutwa nzima na kuondoka kesho yake.
Tulipata hoteli nzuri,tulikula chakula ile roho inapenda na soda na kwenda kulala kwa ahadi ya kesho kwenda kuzunguka mjini tuone ulivyo.asubuhi tukapata breakfast ya nguvu na kutoka kuelekea mjini kwa miguu ili tuufaidi mji.
Jiji la Lusaka ni zuri na liko bize ingawa watu walikuwa wanakatazwa kunywa mchana na serikali lakini bado wanaume wengi mchana walikuwa wanalewa kwa raha zao.tulipagawa tulipoona supermarket zilizojaa vyakula vya aina mbali mbali wakati Bongo kila kitu kwa foleni!  Maduka ya viatu ya bata toka sandal hadi viatu vya ngozi ya kupindua!
Tulizunguka mjini mpaka jioni tukarudi hotelini kujitayarisha kwa safari ya kesho yake…..

Nini kitatokea katika safari ya kwenda Angola?
Usikose kufuatilia sehemu ijayo ya mimi na Angola.




Chapisha Maoni

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Mpya zaidi Nzee zaidi