SEHEMU
YA NNE;
Tulizunguka
mjini mpaka jioni tukarudi hotelini kujitayarisha kwa safari ya kesho yake…..
Hii
ni hadithi ya maisha yangu ninayoiandika
mimi mwenyewe.
Susan
natasha humba.
Sasa endelea na sura ya tano ya mimi na
Angola……
Siku iliyofuata tuliwasili katika uwanja wa ndege wa Lusaka, ilikuwa ni
saa 8 mchana na siku hiyo kulinyesha mvua kubwa sana kiasi tukaanza kupata
wasiwasi kama ndege itafanya safari maana zingine kadha zilikuwa
zimeshafutwa.tulikaa airport tukisubiri hatima yetu kwa masaa hadi tuliposikia
tangazo la kuingia ndani ya ndege.
Tuliingia ndani ya ndege
ya kirusi Aeroflot
na kupaa mawinguni tayari kwa safari ya
Angola, na kuwasili saa 2 usiku na kupokelewa na afisa wa ubalozi na kutupeleka
katika nyumba tuliyofikia ambayo kumbe ilikuwa ni hapo hapo ubalozini.
Ubalozi
wa Tanzania ulikuwa katika barabara ya silver de porto ukiwa katika Jengo la ghorofa tano, chini ni ubalozi na
juu ni makazi ya wafanyakazi wa ubalozi.
Kama kawaida utalitambua kwa kuona bendera niipendayo ya taifa letu
ikininginia ingawa ilikuwa imechoka na kupoteza uzuri wa rangi zake!
Tulipelekwa moja kwa moja ghorofa ya tatu na kutua mizigo yetu.
Kwa
vile ilikuwa usiku tulijipangia vyumba na kulala moja kwa moja.
Mwaka
1980 tulianza rasmi ukazi katika nchi ya
ugeni.
Angola
nchi ambayo kwa huku kwetu kabla hatujaondoka tuliijua kama ni nchi ya
Augustino Neto iliyotawaliwa na wareno kwa miaka mia tano na kufanya lugha ya
taifa kuwa kireno pia inatawaliwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa lugha
nyepesi yaani amani ilikuwa ni msamiati mgumu kueleweka.
Magaidi
wakiongozwa na Mwasi Savimbi walikuwa wanaisumbua sana serikali ya Angola kwa kupigana vita vya
msituni kwa miaka kadhaa.
Sasa
nakupa mtazamo wangu nilipofika Luanda,ambao ni mji mkuu wa Angola.kwanza ni amani tupu wala huwezi jua
kama kuna mtu anatumia risasi mahali Fulani ili aishi. Rais ni Eduardo dos Santos, ni nchi nzuri
iliyotawaliwa na majengo mengi ya ghorofa
na nimejitahidi kila ninapopita nione kama kuna nyumba ya udongo
sikuwahi kuiona zaidi ya nyumba za chini chache. Ujenzi wa nyumba zao wanatumia milango mingi
kama kiunganishi cha chumba na chumba unaweza kukuta sehemu inayotakiwa kuwa na
mlango mmoja wao watajenga mitatu!
marmar za ukutani ni jambo la kawaida katika kuta za nyumba zao.
Luanda
iko pembezoni mwa bahari ya Atlantiki inayosifika kwa samaki wengi na watamu
huko niliwaona samaki wanaoitwa Kashushu
ni samaki pendwa watamu zaidi ya sato maana kwangu sato ni samaki pendwa.kuna
sardina na karapau achilia mbali kamba na kambakoche wanaopatikana kwa wingi,
kwa wiki tulikuwa tukinunua kiroba cha samaki mpaka nikawa napika sambusa za
samaki kila mwishoni mwa wiki! Maana
usipomaliza kiroba hiki kitakutana na kingine cha wiki ijayo, kuna samaki
maalum kwa ajili ya kuchoma tu upo hapo?
Kwenye
hiyo pwani kuna sehemu ambayo ardhi imeingia baharini wenyewe wanaita ilha
(tamka ilya) pana pendeza sana na hiyo sehemu haina kazi nyingine zaidi ya watu
kwenda kushuhudia jua linavyozama tu!
(sunset)
Kwa
upande mwingine wa bahari kuna hoteli nzuri iitwayo Panorama ukiiangalia kwa
woga unaweza kudhani iko ndani ya bahari na pia upande mwingine kuna matanki
makubwa ya mafuta ya petrol.
Usafiri
wa mabasi na sikuwahi kuona taxi labda kwa vile sikuwa nazihitaji! Na kwa upande wa daladala sikuwahi kupanda basi hata mara moja hivyo
siwezi kuelezea adha wanazozipata kama za madaladala yetu hapa.
Cha
ajabu hakukuwa na maduka yanayayouza nguo,chakula wala vifaa muhimu vya
matumizi ya kawaida.bado ile hali kama ya bongo tulipoondoka ya kufunga mikanda
ilikuwa inafanana tofauti tu ni wale wako vitani,kwa sisi wageni wa nchi za nje tulikuwa na duka la
madiplomat, Angodiplo (Angola diplomats)
Huko
ndiko tulikokuwa tukinunua mahitaji ya
vyakula na kwa upande wa nguo ,viatu na mafuta ya kupaka inabidi uagize
uingereza au marekani kwa kutumia
catalogue (vitabu maalum vinavyouza vitu kwa kuagizia) unachagua
unaagiza kisha wanakuletea gharama unazotakiwa ulipe ikiwemo na usafiri unatuma
pesa kupitia benki na baada ya wiki 3
wanakuletea unaaenda kuchukua airport
ambako kuna urasimu mkubwa ukizubaa mzigo wako unaweza kukaa hata miezi
lakini nilijilazimisha wanijue idara zote inakopita mizigo yetu na nilijulikana
fasta hivyo ikawa nikipata tu invoice ya mzigo asubuhi nasema zege halilali ntanengeneka
hadi jioni narudi na mzigo.chezea Natasha wewe!
Domo
mali yangu silipii vat!
Kitu
kingine kilichonishangaza ni kuona wanawake wengi wanavaa nguo nyeusi kila
ukitembea mtaani nikauliza kulikoni?
Nikaambiwa
hao wanavaa hivyo wamefiwa na waume zao vitani.
“Mungu
wangu mbona wengi!
Katika
kundi la wanawake kumi,saba wote wamefiwa!
Kiingine
ni kuona vijana wengi wakiwa wamekatwa ama miguu ama mikono! Kuuliza kisa eti
ni vita!
Kumbe
vijana wakifika miaka 18 ni lazima waende
vitani baada ya miaka miwili anarudi ama mzima ama kilema ama harudi
kabisa! Utawaonea huruma siku ya matibabu ilikuwa alhamisi maana tulikuwa
tunakaa karibu na hospitali ya jeshi hivyo utayaona makundi ya vijana kumi hadi ishirini kila baada
ya muda yanapita na mbaya zaidi wote wamekatwa ama kiungo
kimoja ama kingine!
Mdogo
wangu Tony aliingizwa shule ya international school inayoendeshwa na wafaransa (Alliance
francaise) ndio ilikuwa shule pekee inayofundisha kiingereza na haikuwa mbali na nyumbani.
Mimi
nikapatiwa kazi ubalozini ya usafi ambayo niliifurahia sana, kazi ni kazi nitake kazi ya maana nimesoma? Hiyo hiyo
ambayo kwanza ilikuwa kama hisani tu toka kwa mheshimiwa Balozi ama sivyo
angeuchuna tu.
Cherrie
akabaki nyumbani na mama akimfanyia fujo.
Neno
la kwanza la kireno kujifunza likawa embaixada nikahisi tu hata kabla sijauliza
kuwa ni embassy yaani ubalozi nikaambiwa
sawa nimepatia likaja la pili ni Bondia nikataka kujibu mi sio Mohamed Ally
lakini ukiwa nchi ya watu usijifanye kimbelembele kujibu vitu maana kila eneo
lina namna yake ya kuzungumza mfano umetoka juani na kiu imekushika ukafika kwa
muangola anaweza kukwambia akupe sumu?
lazima utakataa hakuna mtu anaependa kufa sio? Lakini kiukweli utashangaa sana ukiona
wenzako wanapewa kinywaji na wewe mate lita yanakutoka kwa kunyimwa.kumbe sumu
kwa kireno ni juice!
Meza
ni meza.kinyentu ni sh. Mia tano wakati huku nasikiaga masela wanasema nyentu
ni mia,camarada ni comrade, Barida kule
ni bariga maana yake tumbo.huku kona ni kona kule ni neno lisiloweza kutamkika
hadharani.
Shega
kule maana yake inatosha, kuna maneno mengine yanafanana na kiingereza hivyo
unaweza kuhisi ni neno Fulani ila hili la bondia ilibidi niwe mpole kuuliza
maana yake kumbe ni Habari ya asubuhi upo hapo?
Kwa
vile nilikuwa nikifanya kazi na pia kuna wafanyakazi wazawa wa pale angola kama
vile dereva sumao (jina hili kwa kiingereza ni simon) baba mtumzima mwenye
asili ya kongo lakini kalowea
Angola kwa msaada wake na
wafanyakazi wa ndani nilifahamu kireno haraka. Kitu cha kuchekesha wananchi wa
kule sio wengi wanaofahamu kiingereza ila usiwatete kwa Kiswahili
tulipoligundua hilo tukawa tunaogopa kuongea hata Kiswahili njiani maana ghafla
anaibuka mtu akikusapoti unachoongea na kukwambia alikulia morogoro au Dar sasa
ole wako uwe umemteta!
Kutokana
na cheo cha baba yangu alikuwa akipokea vijana wageni wanaojitosa kwenye kazi
ya ubaharia wakidhani kwa vile Luanda kuna bahari basi ni rahisi kupata kazi
kwenye meli….
Je?
Vijana hawa watafanikiwa kupata meli au
kuwin maisha?
Hayo
na mengine mengi utayapata katika sehemu ya sita ya mimi na angola.