Mchakato wa Tuzo za Filamu Nchini Wazidi Kuimarisha Tasnia ya Filamu


 Na Mwandishi wetu

Tuzo za filamu nchini zinaendelea kupamba moto kwa hatua mbalimbali kukamilika kwa mafanikio makubwa.

kwa zoezi la uwasilishaji tuzo, linatarajia kufikia tamati Tarehe 31 ya mwezi huu, ili kupisha mchujo wake.

akitoa maoni yake kuhusiana na tuzo hizo, mwenyekiti wa TDFAA Iringa, Ndugu Khamis Nurdin Amesema kuwa Uwasilishaji na Upokeaji wa Tuzo za Filamu Nchini ni hatua muhimu katika kukuza na kuendeleza tasnia ya filamu nchini.

“Chini ya usimamizi wa Bodi ya Filamu, mchakato huu huimarisha heshima na hadhi ya wasanii, huku ukitambua ubunifu, ubora na mchango wao katika sekta ya burudani.” alisema Nurdini

Mwka huu, mchakato rasmi wa usaili unahusisha matumizi ya teknolojia mabapo mshiriki anatuma kazi yake mtandaoni (Online) kwa mfumo maalum wa tovuti kwa anuani ya www.taffafestival.or.tz/tuzo ili kujisajili na kuwasilisha filamu zao

“Mfumo wa kitaalamu wa uteuzi, upimaji na utoaji wa tuzo unahakikisha uwazi, usawa, na uhalali wa matokeo.”

akifafanua kuhusiana na fursa za kimaendeleo, Amesema kuwa tuzo hizo ni ishara ya ukuaji wa sekta ya filamu Nchini kwani fursa zinajionesha wazi, hata kama hazijashikiwa mabango

“kuwa na Tuzo imara kunachochea ushindani wa kimaendeleo, kuvutia wawekezaji, na kuongeza hamasa kwa wasanii chipukizi. Kwa ujumla, Bodi ya Filamu inapoweka taratibu na vigezo vya uwazi, hujenga imani kwa wadau na kuimarisha nafasi ya filamu za Tanzania katika soko la kitaifa na kimataifa.” aliongezea MwenyekitI huyo

Tangu kuanza kwake mwaka 2021, mwamko umekuwa ukiongezeka katika kila tamasha, na kualika wataalamu wengi zaidi wa kitaifa na kimataifa

 

Chapisha Maoni

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Mpya zaidi Nzee zaidi