Filamu ya “My Son” kuoneshwa 'bure' jijini Dar es salaam


 
Na Charles Mkoka

Baada ya kufanya vizuri kwenye Tamasha na Tuzo za Filamu Tanzania (TAFFA) kwa kutwaa tuzo ya Filamu Bora ya Mwaka 2025/26 pamoja na tuzo nyingine tano, My Son sasa inakuja na experience mpya kwa mashabiki na wadau wa filamu kupitia tour maalum ijulikanayo kama “My Son: Behind The Screen Tour”.

Tour hiyo inalenga kuwapa watazamaji nafasi ya kipekee ya kuingia ndani ya safari halisi ya utengenezaji wa filamu hiyo kuanzia hatua ya wazo, maandalizi, utayarishaji hadi usambazaji wake.

Kupitia tukio hilo litakalofanyika Russian House, mashabiki wa filamu watapata nafasi ya kushuhudia filamu ya “My Son”, kushiriki mjadala wa wazi na waigizaji pamoja na watayarishaji wa filamu hiyo, lakini pia kujifunza changamoto na mafanikio yaliyojificha nyuma ya pazia la kazi hiyo iliyotikisa mwaka huu.

Waandaaji wa tukio hilo wanasema lengo si kuonyesha filamu pekee, bali kuanzisha mazungumzo mapana kuhusu ukuaji wa tasnia ya filamu Tanzania, storytelling ya kisasa pamoja na namna kazi za Kitanzania zinavyoweza kufikia hadhira ya kimataifa.

“My Son” imeendelea kutajwa kama moja ya filamu zilizofanikiwa kuvutia attention kubwa kwa mwaka huu kutokana na ubora wa simulizi, uigizaji pamoja na namna ilivyoweza ku-connect na audience wa kizazi cha sasa.

Tukio hilo litafanyika Juni 12 jijini Dar es Salaam na kiingilio kitakuwa bure kwa wote watakaotaka kushiriki.

Chapisha Maoni

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Mpya zaidi Nzee zaidi